​WAZIRI MKUU WA TANZANIA MH KASSIM MAJALIWA APOKEA SH. MILIONI 5.6 ZA MADAWATI

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watumishi wa umma nchini wawe wabunifu katika kusaidia kutafuta vyanzo vya mapato kwenye jamii inayowa...

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watumishi wa umma nchini wawe wabunifu katika kusaidia kutafuta vyanzo vya mapato kwenye jamii inayowazunguka.

Ametoa wito huo leo (Jumanne, Februari 14, 2017) ofisini kwake mjini Dodoma mara baada ya kupokea mchango wa sh. milioni 5.6 kwa ajili ya kununulia madawati 70 kutoka kwa watumishi wa TAMISEMI – Dodoma.

Amesema ubunifu huo uliofanywa na watumishi wa TAMISEMI, ni mfano mzuri wa kuigwa na watumishi wengine nchini kwani utaisaidia Serikali kuleta maendeleo.

“Hii ni mara ya tatu kwa TAMISEMI kuchangia huduma za jamii kwenye maeneo mbalimbali nchini… lakini pia niwashukuru kwa kuchagua jimbo la Ruangwa kuwa miongoni  mwa maeneo ambayo ni wanufaika wa mchango wenu,” amesema.

“Mchango huu ni mkubwa na utasaidia mikondo miwili kwa shule za sekondari. Tunahitaji kupata mawazo mapya kama haya, na tunahitaji wafanyakazi wengine wajifunze kutoka TAMISEMI,” amesema.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi mchango wao, kiongozi wa ujumbe ulioenda kuwasilisha mchango kwa Waziri Mkuu, Bw. Filbert Rwakilomba amesema lengo lao ni kuchangia madawati 100 lakini wameamua kutanguliza mchango wa madawati 70 na baada ya siku mbili watakabidhi mchango wa madawati 30 yaliyobakia.

Bw. Rwakilomba ambaye anaongoza kamati ya watu 30 ambao ni watumishi kutoka idara tofauti za Ofisi ya Rais TAMISEMI Dodoma, amesema wametoa mchango huo kama ishara ya kuenzi kazi aliyoifanya Waziri Mkuu Majaliwa wakati akiwa Naibu Waziri (TAMISEMI – Elimu).

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

    L. P. 980,

DODOMA.

JUMANNE, FEBRUARI 14, 2017.


COMMENTS

Name

kimataifa,1,Mlipuko,1,mtandao,1,teknolojia,1,
ltr
item
BONGO DONE: ​WAZIRI MKUU WA TANZANIA MH KASSIM MAJALIWA APOKEA SH. MILIONI 5.6 ZA MADAWATI
​WAZIRI MKUU WA TANZANIA MH KASSIM MAJALIWA APOKEA SH. MILIONI 5.6 ZA MADAWATI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiSwyokHZb5ImMFAquykLZrs-AboqyL-CoyQ79vVeEuFZvipMw74dioJqu_QpJ_hKecZ-aYMh4IJKDRqBVKEakSPzc0wVwhNRSFD6jM7apjWQIv88XVWw3_SqI-rygdLbEWJSHnLVm8OYgt/%20cursor:%20pointer;
BONGO DONE
https://bongodone.blogspot.com/2017/02/waziri-mkuu-wa-tanzania-mh-kassim.html
https://bongodone.blogspot.com/
https://bongodone.blogspot.com/
https://bongodone.blogspot.com/2017/02/waziri-mkuu-wa-tanzania-mh-kassim.html
true
5217992609549716446
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy